Wednesday, April 10, 2013

Shule Mkweche Kuliko Zote! Lakini imefaulisha zaidi ya 75% ya Styudentsi wake...




"Shule hii inaitwa Dumanang primary school, ipo katika kijiji cha lukale wilaya ya Meatu, ambapo kutoka Meatu mjini hadi kijijini hapo ni km 110.
Hii ni shule ambayo inafundisha jamii ya watoto wa Kitaturu.
Shule hii ilifanikiwa kufaulisha watoto saba kati ya kumi kwenda sekondari ambapo wanne wakiwa wakiume na wakike watatu, lakini kwa bahati mbaya, watoto watatu walipewa mimba wakiwa sekondari shule za mjini.
Kwa bahati mbaya mmoja wao alifariki katika harakati za kutoa mamba.
Hii imepelekea jamii ya kitaturu kuomba kuletewa sekondari karibu na makazi yao, kufuatia wao kuishi polini, Lakini pia wameomba kuboreshewa shule kutoka kwenye shule ya miti na kwenda katika shule ya block, ambapo kwa nguvu zao tayari wamenza maandalizi.
Shule hii kama inavyoonekana hapo juu,  madarasa yametenganishwa na miti unayoiona katikati kwa ndani. 
Ubao ni mmoja ambao unafindishiwa darasa la kwanza na kuhamishwa darasa la pili hadi la saba kwa ubao huo huo mmoja.
Balaa linakuja, pale ambapo mvua ikinyesha hakuna masomo.
Shule ina walimu watatu, wakike wawili na wakiume mmoja, wanafunzi kuanzia darasa la kwanza hadi la saba wapo 120.
Waheshimiwa naomba kuwasilisha!!"

2 comments: